YAHAYA (MKE WA MTU)

Nasikia mke wa mtu ni digital,
Analogy hakina tena,
Mke wa mtu ni moto,huuotwi kwa mstari chunguza vyema,
Kaa chonjo kada nakupa tu tahadhari mapema,
Jana yahaya katembezwa uchi toka sinza mpaka ubungo mataa,
Watu wanashangaa,kweli mke wa mtu kazua balaa,
Mwanzo,Skendo zimevuja kita,jimama linatembea na jamaa,
Na jamaa,na jamaa ni mwana wangu balaa,
Yani Mwana tumekuwa wote kitaa,
Mwana mwenye ni yahaya muuza sukari guru,
Nikamvutia wanya yahaya,akagoma akataa,
Nakaona ,poa yawezekana,wanamsingizia kachaa,
Zikapita siku ,mwenzi ,mwaka yahaya hapatikani kitaa,
Kapigwa selo ya mapenzi,na jimama,mke wa mdosi wa kitaa,
Mke kageuga sugu,kamiliki jimbo kabisa kwa jamaa,
Akamnunulia nyumba na gari ya kutembelea kachaa,
Pesa haisihi mfukoni  yahaya akageuka bili geti wa mtaa,
Kweli ziki mwana haramu,leo pesa inamnenepesha kachaa,
Makeke yalizidi kitanda,yakamchanganya jimama balaa,
Maujuzi ya kitaa,zikamfanya mke wa mtu azidi mwange chapa,
Penzi likavuka mpaka wakaanza kufaya hadharani,
Taarifa zikafika mdosi,mkewe anatembea na fala mmoja mtaan,
Kikao cha dharula kikakaa,Mdosi akatoa silaha na chapa,
Pesa nyingi balaa milioni 200, atakaye mkamata  kachaa,
Msako ukanza kitaa,wakwanza mimi ,mawela ,ghetto wa kazagaa,
Wakanipigwa maswali yupo wapi kachaa,yupo wapi yahaya, nyoka,?
Mmoja akanishikia bastola kichwani, ile na guna akapiga moja hewani,
msako ukavuka sinza,mbezi,mpaka huko tegeta corner,
kila mtu anamsaka yahaya maana kashageuka  pesa,
yahaya wa sinza ,fala leo amegeuka pizza,ghafla
yahaya akaonekana vingunguti kwenye mabucha ya mbuzi,
wanaa  kumuona tu  wakapiga miluzi,
yahaya kuona so ikabidi ajisalimishe,
huu ndo ulikuwa mwisho wa muuza sukari guru,
leo anashinda majalalani yahaya kageuka kichaa,
mdosi kampiga sindano,nauoza taratibu kachaa,
kweli ni nimeamin mke wa mtu  ni balaaa,
ukitembea nae jiandae tu ipo siku utashangaa,
sure utashanga,majitu wanalishasema,
siku ya siku utakojoa dagaa,utachaa,kama yahaya alivyofubaa..

mwili nusu umeshaoza,anasubiria kufa kachaa..